emblem

Energy and Water Utilities Regulatory Authority Consumer Consultative Council

EWURA CCC

News

Baraza lafunda vijana 150 Lindi


Kamati ya watumiaji ya EWURA CCC mkoani Lindi, imeshiriki kwenye maonesho ya wiki ya vijana kitaifa na kuelimi­sha zaidi ya wadau 150 kuhusu masuala mbalimbali yanayohu­su huduma za nishati na maji zinazodhibitiwa na EWURA.

Akiongea wakati wa maone­sho hayo yaliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Mpilipili, Manispaa ya Lindi kuanzia tarehe 08 hadi 14 Ok­toba 2019, Mwenyekiti wa Ka­mati ya watumiaji ya Mkoa wa Lindi Bibi Angelina Murangira, alitaja malengo ya ushiriki wa Baraza katika maonesho hayo kuwa ni pamoja na kuitangaza EWURA CCC, ili itambulike mi­ongoni mwa wadau na waitumie kunapokuwa na uhitaji.

Alitaja malengo mengine kuwa ni pamoja na kukutana na wadau ambao siyo rahisi ku­wafikia kwa kutumia njia zingine, kujibu maswali na kutatua chan­gamoto zinazoibuliwa na wadau.

“Matukio kama haya ni muhimu sana kwa taasisi kama EWURA CCC kushiriki kwa kuwa tunawafikia wadau muhimu mno ambao tusingeweza ku­wafikia kwa kutumia njia nyingine yoyote ile,” alisisitiza Bibi Murangira.

Alisema maonesho ya wiki ya vijana 2019, yamekuwa ni mi­ongoni mwa maonesho ambayo yamepata mwitikio mkubwa wa wadau kutembelea banda la Baraza na kwa kupitia maone­sho hayo, Baraza limepata fursa nzuri kuelimisha na kujibu hoja zilizojitokeza.

“Vijana wengi walihoji tatizo la uhaba wa maji kwenye mae­neo mengi ya Manispaa ya Lindi. Bahati nzuri tuliwaelimisha mi­pango ya LUWASA ya kuhakiki­sha huduma ya maji inawafikia wananchi wengi zaidi,” alieleza Bi. Murangira.

Alisema njia zilizotumiwa na Kamati yake katika kutoa elimu kwa makundi ya vijana ni pamoja na utoaji wa elimu kwa kila kundi kama darasa, na ma­jadiliano.

Bi Murangira aliyataja mae­neo ya uelimishaji yaliyotolewa wakati ya maonesho hayo kuwa ni pamoja na elimu kuhusu uwe­powaEWURACCC namajukumu yake, haki na wajibu wa mtumia­ji, matumizi sahihi ya huduma na namna ya kuwasilisha na kushughulikia malalamiko.

“Ilikuwa ni muhimu kuwaeli­misha vijana na hata wadau wengine waliotembelea banda la EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wao kwa kuwa, kufanya hivyo kunawaandaa kuwa na uwezo wa kudai haki hizo zin­apokiukwa,” alieleza bi Muran­gira na kuongeza kuwa elimu kwa mtumiaji inakiweka kizazi cha sasa kwenye nafasi nzuri ya kuchangia katika kuboresha huduma za nishati na maji.

Nao baadhi ya wadau walio­tembelea banda hilo walionesha wazi kuridhishwa na elimu wali­yoipata na kuahidi kuelimisha ndugu na marafiki zao ili kuwa na makundi ya watumiaji yan­ayoweza kujisimamia na kupiga­nia haki zao.

Kamati ya EWURA CCC mkoani Lindi imejipanga kuyafikia makundi mengine mengi katika jamii kwa kupitia mikusanyiko, makongamano na semina ili kuelimisha na ku­hamasisha umuhimu wa ushiriki wao katika uboreshaji wa hudu­ma za nishati na maji mkoani humo.

Na Jumbe Kawambwa